Monday, April 4, 2011


Mtumishi wa Mungu Furaha Willy akihubiri injili ya YESU KRISTO aliye hai siku ya kwanza ya mkutano.

Umati wa watu wakinyosha mikono yao juu kwa ishara ya kukabidhi maisha yao kwa YESU.

Mungu aliokoa watu mbalimbali katika mkutano na hawa ni baadhi ya watu walioamua kumpa YESU KRISTO maisha yao.Kwani neno la Mungu linasema YESU ndiye njia ya kweli na uzima, na mtu haji kwa baba pasipo njia ya YESU.yOH 14:6


Watumishi wa Mungu wakisikiliza mahitaji ya watu na kuwaombea.

Watumishi wa Mungu wakifanya maombezi kwa watu wenye shida na mahitaji mbalimbali.

Baadhi ya watu wakimsifu Mungu akiongozwa na Mwimbaji wa nyimbo za Injili Past.Beni


Makutano wakimwabudu Mungu aliye hai..

Wtumishi wa MUNGU wanaTALITHA KUMI wakiwa jukwaani wanamsifu Mungu wakiongozwa na Joshua Silomba(katikati).


Baadhi ya viongozi wa TALITHA KUMI wakiwa katika mkutano.

Baadhi ya watu waliohudhuria mkutano wakifuatilia kwa makini mahubiri.

Wapigaji wa muziki na mafundi mkitambo katika mkutano.


Baadhi ya watumishi wa Mungu wakliokuwa wakihudumu katika mkutano Arusha wakiwa katika jukwaa.

Mtumishi wa Mungu Deogratius Njeni akiomba kwa ajili ya mtumishi wa Mungu,


Mtumishi wa MUNGU Onjeni Njeni akihubiri wakati wa mkutano wa TALITHA KUMI huko ARUSHA

Wakati wa sifa watu wakijiachia vyema mbele za Mungu wao.maana hakuna astahiliye kusifiwa.

Mtumishi wa Mungu Muimbaji mwana TALITHA KUMI Frank Mbunda akiongoza ibada ya sifa.

Baadhi ya waumini wa kanisa la Siwandeti wakijibwaga wakati wa kipindi cha kumsifu Mungu.

Mtumishi wa Mungu Onjeni Njeni akifundisha maneno ya Mungu katika Ibada kubwa iliyofanyika katika kanisa la Siwandeti jijini Arusha.


Baadhi ya watu wliohudhuria katika ibada kanisani siku ya jumapili,ambayo ni siku ya kwanza ya mkutano.


Baadhi ya mafundi mitambo na wapiga vyombo vya muziki ambao ni watenda kazi ndani ya TALITHA KUMI.

baadhi ya watu wakimsifu Mungu katika mkutano wakati wa sifa.

Baadhi ya waimbaji wakimsifu Mungu siku ya kwanza ya mkutano, akiwemo Mwimbaji binafsi ENJOLIT KIMARO(katikati)

Sehemu ya umati wa watu waliohudhuria katika mkutano mkubwa wa Injili siku ya kwanza huko Siwandeti Arusha.




Mchungaji kiongozi wa kanisa la Jesus healing Siwandeti Arusha mama Maria Shauri.


Watumishi wa Mungu Furaha Willy kutoka kushoto ambaye ni Katibu wa huduma ya TALITHA KUMI,na Onjeni Njeni ambaye nimwezeshaji mkuu (COORDINATOR) wa huduma ya TALITHA KUMI.

Mtumishi wa Mungu Edward Emanuel ambaye ni Mwenyekiti wa huduma ya TALITHA KUMI akiwa anamkaribisha mtumishi aliyeandaliwa kwa ajili ya neno siku hiyo.

Mchungaji na mama mchungaji Shauri,wenyeji wa kanisa la Jesus healing Siwandeti Arusha, ambapo mkutano Mkubwa wa Injili ulifanywa na huduma ya TALITHA KUMI.

VITU VYA KICHAWI VIKITEKETEZWA NA WANATALITHA KUMI HUKO ARUSHA.

MKUTANO MKUBWA ULIOFANYIKA ARUSHA TAR 6/3-13/3,2011

Mkutano huo uliofanyika Arusha kijiji cha Siwandeti wilaya ya Arumeru,ulihudhuriwa na watu wengi ambapo pia mungu alifanya mambo makuu, aliponya, aliokoa na mengine mengi Mungu wetu aliye hai alifanya.

Saturday, April 2, 2011

VIONGOZI WA TALITHA KUMI

Mkurugenzi wa huduma ya TALITHA KUMI,Mtumishi wa Mungu Deogratius Njeni kutoka Mkoani Mbeya Tanzania,ambaye ni mwanazuoni wa Chuo Kikuu Cha Dodoma mwaka wa tatu(mwisho) akichukua shahada ya Utawala wa Umma (BA,PUBLIC ADMINISTRATION).Huyu ndiye Mungu aliyempa kubeba maono ya huduma ya TALITHA KUMI

Friday, April 1, 2011

WAHUDUMU WA TALITHA KUMI

Mhudumu wa TALITHA KUMI anatakiwa awe na sifa zifuatazo:
  • Awe amempokea YESU KRISTO kama Bwana na Mwokozi wa maisha yake.
  • Awe tayari kujitoa kwa ajili ya YESU KRISTO na si Mwanadamu.
  • Awe amesajiliwa ndani ya TALITHA KUMI.
  • Awe tayari kufuata Katiba na taratibu za TALITHA KUMI

WALENGWA WA TALITHA KUMI

Watu wote bila kujali elimu,dini,kabila,jinsia,rangi na vyeo{Warumi 1:16}

NAMNA TALITHA KUMI INAVYOFANYA HUDUMA

TALITHA KUMI inafanya huduma kupitia njia mbalimbali kam vile:
  • Semina za neno la Mungu ndani na nje ya kanisa.
  • Mikutano ya Injili
  • Warsha mbalimbali
  • Mahubiri ya mitaani.
  • Mahubiri ya nyumba kwa nyumba.
  • Kutoa ushauri na kufanya maombezi kwa watu wenye mahitaji mbalimbali

    MALENGO YA TALITHA KUMI

    1. Kutimiza neno la kinabii katika mpango wa YESU KRISTO wa kulijia na kulirejeza kanisa lake.
    •    Kuleta uamsho wa kanisa ulimwenguni kote kwa maana wakati wa Bwana na jeshi lake umetimia katika hatua katika hatua za mwisho za unyakuo wa kanisa .(Yoeli 1:15)
         2.Kuinua vipawa vya Kimungu kati ya vijana kwa matabaka yote 

        3. Kukutana na jamii za watu mbalimbali  wenye mahitaji maalum kama wagonjwa,walemavu,waathirika 
            wa UKIMWI na madawa ya kulevya.  

       4.  Kutoa ushauri na kufanya maombezi kwa watu wenye mahitaji mbalimbali

    MAONO YA TALITHA KUMI

                TALITHA KUMI ina maono ya kufikisha Injili ya YESU kwa watu waliopo vijijini na mijini na kuwafungua waliofungwa na vifungo mbalimbali vya kiroho na kimwili {Isaya 61:1-2}

    MAANA YA TALITHA KUMI

         Ni huduma ya uamsho na urejesho wa vijana na watu wote.TALITHA KUMI ni neno la Kiebrania lenye maana ya KIJANA INUKA{Marko 5:41} ambalo lilitumiwa na YESU akionyesha wakati wa uamsho na ufufuo juu ya kanisa lake kama alivyoahidi katika kitabu cha Amosi 9:11,siku hiyo nitaiinua tene masikani ya Daudi iliyoanguka na kuziba kuziba mahali palipo bomoka,nami nitayainua magofu yake na kuyajenga kama siku za kale.

    KUHUSU TALITHA KUMI

           Ni huduma ya uamsho iliyoanzishwa mwaka 2007 mkoani Mbeya Uyole Tanzania,chini ya mwasisi wake Mtumishi wa Mungu Deogratius Njeni ambaye alipewa maono na Mungu wa mbinguni aliye hai, ambaye ndiye aliyepokea  wito wa huduma hii akishirikiana na wachungaji wa kanisa la Pentekoste Revival Church,akiwemo mchungaji Odiah Njeni na vijana wengine.
         Huduma hii ilipata mashiko zaidi mwaka 2010 katika Chuo Kikuu Cha Dodoma ambapo wanazuoni wengi walijiunga na huduma hii,na kuanza kumtumikia Mungu kwa kasi kubwa kwa kufanya huduma za mikutano ya nje,semina za ndani,ushuhudiaji wa nyumba kwa nyumba na mahubiri ya mitaani sehemu mbalimbali za nchi ya Tanzania na Mungu alionekana kitenda mambo makuu sana.